Showing posts with label Leon Bahati. Show all posts
Showing posts with label Leon Bahati. Show all posts

Friday, December 9, 2011

Spika, Katibu wa Bunge wapingana posho

venance.chadema@yahoo.com

 Send to a friend
Thursday, 08 December 2011 21:04
Spika Anne Makinda

SAKATA la nyongeza ya posho za wabunge sasa limegeuka vita baina ya watendaji wakuu wa taasisi hiyo ya kutunga sheria; Spika Anne Makinda na Katibu wake, Dk Thomas Kashililah.

Hali hiyo inaonekana baada ya Dk Kashililah jana kuendelea kusisitiza kuwa kauli yake kwamba posho hizo hazijaanza kutolewa kwa kuwa Rais Jakaya Kikwete hajasaini, bado ni sahihi na kuahidi kuweka mambo hadharani akirejea nchini kutoka jijini London.Dk Kashililah alitoa kauli hiyo jana alipokuwa akizungumza na gazeti hili akiwa London Uingereza kuhusu mgongano wa kauli na msimamo kuhusu posho hizo, uliojitokeza baina yake na Spika Makinda.

“Mimi ni Mtendaji Mkuu wa Ofisi ya Bunge. Na ninapozungumzia jambo nina uhakika na kile ninachokizungumza kwa kuwa najua wajibu wangu,”alisema Dk Kashililah.

Alisisitiza kuwa kauli aliyoitoa awali, inatokana na kile alichokuwa akikifahamu kwa mujibu wa mamlaka yake ya kiutendaji na madaraka aliyonayo kwenye ofisi hiyo ya Bunge.

Dk Kashililah alisema hana wasiwasi na kauli yake na hivyo akaomba apewe muda kwa kuwa wakati mwingine siyo vyema kuzungumzia jambo linalohusu ofisi akiwa nje ya nchi.

“Njoo ofisini (Jumatatu) nikisharudi  nitalielezea vizuri jambo hilo,” alisema

Monday, July 18, 2011

Shellukindo ailipua Wizara ya Ngeleja .

venance.chadema@yahoo.com

Monday, 18 July 2011 21:36
MBUNGE wa Kilindi (CCM), Beatrice Shellukindo amelipua bomu Bungeni akimtuhumu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, David Jairo, kwa kutumia zaidi ya Sh 1 bilioni kwa ajili ya kutoa rushwa kwa watu mbalimbali ili bajeti ya wizara hiyo iweze kupitishwa na Bunge.Tuhuma hizo nzito zinakuja kipindi ambacho tayari Wabunge wa Kamati ya Nishati na Madini wakiwa wameibua tuhuma kama hizo za baadhi ya wajumbe kutaka kuhongwa na maofisa wa wizara hiyo, ili kurahisisha upitishaji wa bajeti ndani ya kamati.

Takriban wiki tatu tangu wabunge wa kamati hiyo kuibua tuhuma

Friday, July 15, 2011

Lowassa: Nimeshtushwa.

 Send to a friend
Thursday, 14 July 2011 22:42

Mbunge wa Munduli, Edward Lowassa akizungumza na waandishi wa habari kwenye viwanja vya bunge mjini Dodoma jana, walipotaka kupata maoni yake kuhusu uamuzi wa Rostam Aziz kujiuzulu nyadhifa zake za ubunge wa Igunga na ujumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM

WAKATI uamuzi wa Rostam Aziz kung'atuka ubunge wa Igunga na ujumbe wa Halmashauri Kuu (Nec) ndani ya chama chake cha CCM ukiibua gumzo kubwa karibu kila kona nchini, mshirika wake mkubwa kisiasa, Edward Lowassa ambaye ni Mbunge wa Monduli ameeleza kushtushwa na tukio hilo.Juzi, Rostam, mmoja wa watu muhimu ndani ya CCM aliyeshiriki vyema katika mtandao uliomwingiza madarakani Rais Jakaya Kikwete mwaka 2005, alitangaza uamuzi mzito wa kung'atuka siasa akipinga kile alichokiita siasa uchwara za baadhi ya viongozi wake.Uamuzi huo mzito wa Rostam uliibua kwikwi na vilio kutoka kwa wapigakura jimboni kwake Igunga, wakiwamo wale waliomchagua kwa vipindi vitatu mfululizo tangu mwaka 1994 ulipofanyika uchaguzi mdogo kufuatia kifo cha aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo, Charles Kabeho. Jana, Lowassa alisema: "Kwa kweli nimeshtushwa, nimesikitishwa...kilichonishtua zaidi ni vilio. Namna wananchi wa Igunga walivyokuwa wanalia na kusikitika."

Hata hivyo, Lowassa ambaye naye amekuwa akitajwa katika orodha ya